Infinix NOTE 11 kuwagusa zaidi wadau wa masuala ya urembo

0
13

Infinix NOTE 11 kuja na kioo aina ya AMOLED na hii kuwa simu ya kwanza kwenye series ya NOTE kuja na aina hiyo ya kioo ambayo sifa yake kubwa kioo hiki ni kutoa picha zenye rangi halisi ya mazingira husika. Infinix ni kampuni ambayo inazingatia zaidi trends za industry mbalimbali kama fashion, tech n.k

Infinix NOTE 11 kuja kuwagusa zaidi industry ya urembo kutoka na aina nzima ya muonekano na sifa za simu hiyo, Infinix NOTE 11 ni simu ya kwanza kwa kampuni ya Infinix kuja na umbo jembembe zaidi na nchi 6.7 AMOLED display FHD.

Kuhusu camera bado haijafahamika ni Megapixel ngapi lakini kwa tunavyofahamu Infinix haijawahi kurudi nyuma Infinix NOTE 10 ilitamba na megapixel 48 na baada ya muda ilikuja NOTE 10 na Megapixel 64 kwa ukuaji huu wa camera basi ni wazi huenda NOTE 11 ikawa na camera kubwa zaidi ya series za NOTE  za awali.

Hizi ni baadhi ya dondoo ambazo zimeonekana kuzagaa kwenye mitandao mbalimbali ya tech kama Tanzaniatech na nyenginezo. Je unaisi ni feature gani nyengine mpya kuja na Note 11 https://bit.ly/3BHedZw?

Tafadhali kaa karibu na @infinixmobiletz kujua zaidi kuhusu simu hii.

 

Send this to a friend