Namna 6 bora za kumuacha mtu katika mahusiano

0
28

Hakuna njia rahisi ya kusema “sikupendi tena” lakini kuna njia za upole za kuachana na mtu ambaye ulimpenda hapo awali ambazo hazitoleta tofauti kati yenu.
Hizi ni njia 6 za kuachana na mpenzi wako uliyewahi kumpenda

1. Usijisikie hatia
Hakuna ubaya au ubinafsi kutaka kuachana na mtu ambaye humpendi tena. Unaweza kujisikia vibaya, lakini sio mbaya. Usijiruhusu kulemewa na hisia za hatia au kujichukia, au kufikiria vibaya kuhusu uamuzi wako wa kukomesha uhusiano wako.

2. Kubali kwamba hakuna njia rahisi ya kutengana
Ukweli ni kwamba hakuna unachoweza kufanya ili kupunguza maumivu ya kuachana. Inaumiza kukataliwa, bila kujali sababu ya kuachana. Na ni vigumu kuacha uhusiano hasa kwa mtu uliyewahi kumpenda hapo awali.

3. Kuwa na ujasiri wa kusema kwaheri uso kwa uso
Mtu ambaye unataka kuachana naye, unatakiwa kumwambia uso kwa uso na pengine kufanya majadiliano kuhusu kwa nini uhusiano huo umekwisha. Usitumie barua pepe, au SMS au mitandao ya kijamii ili kukatisha uhusiano wa mapenzi, hata kama mmekuwa pamoja kwa wiki au miezi michache tu.

4. Chagua wakati na mahali sahihi
Usitengane na mpenzi wako katika Siku ya Wapendanao, baada ya mazishi ya familia, mkesha wa mwaka mpya, kwenye hafla kubwa za umma, na kabla au baada ya siku za kuzaliwa. Subiri wakati sahihi.

5. Anza mazungumzo kwa njia chanya
Zungumza na mpenzi wako unayetaka kuachana naye kwa upole kwa kuthamini na kuheshimu hisia zake na kueleza mazuri yaliyotokea wakati wa mahusiano yenu. Hii haitaondoa maumivu yote ya kutengana, lakini baadaye labda itamfanya ajisikie vizuri kidogo.

6. Mueleze kwanini mnaachana
Hii ndio sehemu ngumu zaidi ya kuachana na mtu, hata ikiwa humpendi tena. Kuwa mwaminifu kunahitaji ujasiri na busara. Kabla ya kuketi na kuzungumza, chukua muda wa kupanga kile utakachosema na jinsi utakavyosema. Usisitishe mjadala huo na usiahirishe mipango yako na maandalizi ya mazungumzo ya kutengana, Kadiri unavyoepuka, ndivyo utashindwa kuachana naye.