Maswali 5 ya kujiuliza endapo unataka kurudiana na Ex wako

0
18

Kuachana kunaweza kuwa kichocheo cha kujifunza pale ulipokosea. Wakati kutengana kunapotumika kama zana ya kujifunzia, kunaweza kukusaidia kubainisha endapo uhusiano huo unaweza kuanzishwa tena na kuwa wenye afya au kuzalisha matatizo.

Unapotafakari kuhusu uhusiano wako, baadhi ya maswali muhimu yanaweza kukupa ufafanuzi wa jinsi ya kusonga mbele au kurudi kwenye uhusiano huo.

Kwa nini mliachana?

Pengine mliachana kwa sababu nzuri au mbaya, kwa hiyo ni muhimu kukumbuka sababu gani ilifanya kuachana kwenu, kwani itasaidia kukupa majibu mazuri na kujua endapo uhusiano huo unaweza kujengeka tena au kutozaa matunda ikiwa mtarudiana. Ikiwa sababu ya kuachana kwenu ni mbaya ni rahisi kusahau na kusonga mbele.

Watu wako wanasema nini kuhusu uhusiano wenu?

Zungumza na watu wako wa karibu walioshuhudia uhusiano wenu. Waulize: “Je!, “Ni nini kilinifanya nisiwe na furaha?”, “Je, unafikiri mtu huyu ni mzuri kwangu?.”

Kupata maoni ya watu kutoka nje hukusaidia kutafakari uhusiano wako kwa uwazi zaidi.

Nini kinahitaji kubadilika?

Wewe au mpenzi wako wa zamani mnahitaji kubadilisha nini ambacho kinaweza kuzuia makosa katika uhusiano huo? (Kwa mfano), Je! Umejifunza kuweka mipaka na kuondoa vikwazo vilivyoharibu uhusiano wenu? Je! Wewe na mpenzi wako wa zamani bado mnapitia hatua zinazopingana? Hatua hii ni muhimu kwani itaamua endapo makosa yaliyopelekea kuvunja uhusiano wenu yanaweza kuondolewa au la.

Je! Ni kwa sababu ya upweke?

Ikiwa unataka kumrudia mpenzi wako wa zamani kwa sababu unasumbuliwa na upweke kwa kuwa baada ya kuachana kwenu hujafanikiwa kupata mtu mwingine, basi hiyo sio sababu nzuri za kurudi nyuma. Lakini ikiwa una furaha, mzima na umegundua tu kwamba alikuwa sehemu nzuri ya maisha yako, hilo ni wazo zuri la kurudiana naye.

Ndiye mtu bora zaidi kwako?

Je! Una uhakika kuwa huyu ndiye mtu bora zaidi kwako? Je! Sifa za mtu huyu zinaambatana na mambo ya msingi ambayo unahitaji katika uhusiano?

Tengeneza orodha fupi ya mahitaji yako bila yeye akilini kisha vuta kumbukumbu na uone ni wapi anaangukia kwenye hiyo orodha kisha utaona ikiwa anafaa.

Baada ya kupata majibu ya maswali haya, sasa unaweza kuamua endapo umrudie au usonge mbele.

Send this to a friend