Hatua 6 za kuzingatia unapoitwa kwenye mahojiano na polisi

0
20

Kuitwa polisi ni hali inayoweza kutokea kwa sababu mbalimbali, ikiwa ni pamoja na uchunguzi wa makosa, kutoa taarifa, au kutoa ushahidi.

Ikiwa unaitwa kwenye kituo cha polisi au kuna haja ya kushughulikia suala na polisi, ni muhimu kuchukua hatua kadhaa ili kuhakikisha haki zako zinalindwa.

Hizi ni baadhi;

1. Kuwa mtulivu: Endapo utaitwa na polisi au kukufuata kwa ajili ya kuambatana nao, ni muhimu kuwa mtulivu na kuheshimu mamlaka yao. Epuka kuwa na majibu ya kukaidi au kuleta fujo.

2. Jua haki zako: Kujua haki zako ni muhimu. Huna ulazima wa kutoa taarifa zozote hadi utakaposaidiwa na wakili wako. Unaweza kuuliza sababu ya wito wao au unaweza kuomba kuwa na wakili wakati wa mahojiano.

3. Jihakikishie usalama wako: Hakikisha una mawasiliano na mtu fulani anayeweza kujulishwa kuhusu hali yako. Ikiwa ni lazima, wasiliana na wakili wako.

4. Chukua taarifa: Ikiwa umefuatwa na polisi, hakikisha unajua taarifa kadhaa kama majina yao, cheo, na kituo wanachofanyia kazi. Pia, weka kumbukumbu ya mazungumzo na tarehe ya tukio.

5. Usisaini kitu bila kuelewa: Ikiwa utaulizwa kusaini chochote, hakikisha unaelewa kikamilifu kile unachosaini. Ikiwa haujui, ni vyema kuomba maelezo zaidi au kupata ushauri wa kisheria.

6. Beba kitambulisho: Inaweza kuwa ni kitambulisho chako cha taifa au leseni ya udereva. Kitambulisho hiki kitasaidia kuthibitisha utambulisho wako.

Send this to a friend