Nchi 10 za Afrika zenye deni kubwa IMF katika robo tatu ya mwaka 2024

0
5

Nchi nyingi zinakabiliwa na changamoto za kiuchumi ambazo mara nyingine husababisha kutafuta msaada kutoka kwa taasisi kama Shirika la Fedha Duniani (IMF), ambapo huchukuliwa kama suluhisho la mwisho kuinua uchumi wa nchi pindi unapotetereka.

Katika hali nyingi, mkopo kutoka IMF unaweza kuwa na faida na hasara, ukitoa unafuu huku ukikusanya deni ambalo linaweza kuwa gumu kulipa. Hali hii inaweza kusababisha matokeo mbalimbali yanayoathiri uchumi wa nchi.

Kiasi kikubwa cha mkopo kutoka IMF kinaongeza mzigo wa deni la nchi. Kusimamia deni hili itahitaji mipango ya kifedha makini, ambayo inaweza kupunguza uwezo wa serikali kusaidia programu za maendeleo na huduma za kijamii ndani ya mipaka yake.

Tanguzi mwezi Julai, Nigeria na Morocco zimetoka kwenye orodha hii, na nafasi zao kuchukuliwa na Cameroon na Ethiopia.

hizi ni nchi 10 za Afrika zenye deni kubwa zaidi kutoka IMF katika robo tatu ya mwaka 2024;

1. Misri: TZS trilioni 27.4
2. Angola: TZS trilioni 8.14
3. Kenya: TZS trilioni 6.9
4. Ghana: TZS trilioni 6.2
5. Ivory Coast: TZS trilioni 6.12
6. DR Congo: TZS trilioni 4.3
7. Afrika Kusini: TZS trilioni 4.1
8. Senegal: TZS trilioni 3.08
9. Cameroon: TZS trilioni 3.07
10. Ethiopia: TZS trilioni 2.9