VODACOM YAWAPA WASICHANA DAR ES SALAAM MAFUNZO YA TEHAMA KUPITIA PROGRAM YA ‘CODE LIKE A GIRL’
Mtaalamu wa mifumo ya kompyuta wa kampuni ya Vodacom Tanzania PLC, Naamini Yonazi akiongea na wasichana wanaofanya mafunzo ya Code like a Girl yanayofadhiliwa na kampuni hiyo kupitia asasi ya dLab jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki ikiwa ni muendelezo wa programu hiyo yenye lengo la kuleta fursa kwa wasichana kujifunza na kukuza ustadi wa kidijitali, ikiwa ni hatua muhimu ya kuhakikisha wasichana wanajikita zaidi katika masomo ya Tehama.
Mkuu wa Idara ya Rasilimali watu, Sorayya Shareef akitoa vyeti kwa wanafunzi walioshiriki katika programu hiyo.
Wanafunzi wakiwasilisha kazi zao.