
Cropped shot of an unrecognizable man leaning on his walking stick
Wengi wetu hatukai tukijiuliza tutaishi kwa muda gani, lakini wastani wa maisha katika nchi una maana zaidi. Ni kiashiria muhimu kinachoonesha jinsi jamii inavyofanya vizuri katika huduma za afya, hali ya maisha, elimu, lishe, na hata uthabiti wa kisiasa.
Kwa ujumla, matarajio ya muda wa kuishi duniani yanatofautiana kulingana na mahali ulipozaliwa. Kwa mujibu wa ripoti ya hivi karibuni ya World Population Prospects kutoka Umoja wa Mataifa, kuna pengo kubwa kati ya mataifa ya kipato cha juu na yale ya kipato cha chini.
Nchi tajiri, zenye mifumo ya afya iliyoendelea, mazingira safi, na miundombinu bora, huwa na wastani wa juu wa maisha ikilinganishwa na nchi masikini ambazo zinakabiliwa na magonjwa na upatikanaji hafifu wa huduma za afya.
Kwa bahati mbaya, Afrika inaongoza kwa kuwa na nchi nyingi zenye wastani wa maisha mafupi. Kati ya nchi 25 zenye wastani mdogo zaidi wa maisha duniani, 24 zipo barani Afrika.
Kwa mfano, wastani wa maisha nchini Nigeria ni miaka 54.6, hali inayotofautiana sana na Monaco, nchi inayoongoza kwa wastani wa maisha, ambako watu huishi kwa wastani wa miaka karibu 87. Hii ni tofauti ya zaidi ya miaka 32.
Hizi ni nchi 10 bora za Kiafrika zenye wastani wa umri mdogo zaidi wa kuishi kwa mujibu wa UN’s World Population Prospect;
1. Nigeria: 54.6
2. Chad: 55.2
3. Sudan Kusini: 57.7
4. Afrika ya Kati: 57.7
5. Lesotho: 57.8
6. Somalia: 59.0
7. Mali: 60.7
8. Guinea: 60.9
9. Benin: 61.0
10. Burkina Faso: 61.3