
Dar es Salaam, Machi 11, 2025 – Benki ya Exim Tanzania imezindua rasmi huduma yake mpya inayojulikana kama Lipa Chapchap, suluhisho bunifu la malipo ya kidijitali ambalo linarahisisha miamala kwa biashara na watu binafsi.
Njia hii ya malipo maarufu kama “Maliza Kirahisi na Lipa ChapChap’ inayowafaa wafanyabiashara, ambayo ni salama na yenye ufanisi, inaimarisha dhamira ya Benki ya Exim kwa uboreshaji wa kidijitali, ubunifu, na ushirikishwaji wa kifedha.
Kwa kutumia Lipa Chapchap, wafanyabiashara na wateja sasa wanaweza kufurahia huduma bora ya miamala iliyo salama na isiyotumia fedha taslimu kwa kuchanganua tu msimbo wa QR au kama wengi tulivyozoea kuiita QR code na hivyo kuondoa hitaji la malipo ya fedha taslimu.
Huduma hii ni bure kwa wafanyabiashara, na kuifanya kuwa chaguo linalovutia kwa biashara zinazotaka kuboresha mifumo yao ya malipo bila kupata gharama za ziada.
Akizungumza wakati wa uzinduzi, Andrew Lyimo, Mkuu wa Huduma za wateja binafsi na wakati kutoka benki ya Exim, amesisitiza maono ya Benki ya Exim kwa uchumi ulioimarishwa kidijitali. Amesema, “Maliza Kirahisi na Lipa Chapchap inadhihirisha dhamira yetu kwa ubunifu na urahisi.
Mkuu wa Idara ya Wateja Wadogo na Kati wa Benki ya Exim, Bw. Andrew Lyimo (katikati) akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi rasmi wa huduma mpya inayojulikana kama Lipa Chapchap, suluhisho bunifu la malipo ya kidijitali ambalo linarahisisha miamala kwa biashara na watu binafsi. Kushoto kwake ni Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano Bw. Stanley Kafu, na Mkuu wa Idara ya Njia Mbadala za Kidijitali, Silas Matoi kutoka benki ya Exim Tanzania. Tukio hili limefanyika leo jijini Dar es Salaam.
Suluhisho hili haliongezi tu ufanisi wa malipo lakini pia linakuza ushirikishwaji wa kifedha kwa kuhudumia kila mfanyabiashara (zikiwemo biashara ndogo na za kati) ikiwa ni njia salama, isiyo na gharama, na inayopatikana kirahisi ya kupokea malipo ya kidijitali papo kwa papo. Lengo letu ni kuunda mfumo wa mazingira usiotumia fedha taslimu ambao unawanufaisha wafanyabiashara na wateja,”.
Kuanzishwa kwa Lipa Chapchap kunaendana na uchumi unaokua wa kidijitali wa Tanzania, kuruhusu biashara kupokea malipo kutoka benki zote na waendeshaji wa mitandao ya simu—kuhakikisha ushirikishwaji na uwezo wa kuingiliana katika majukwaa ya kifedha.
Naye, Silas Matoi, Mkuu wa Njia Mbadala za Kidijitali, amesisitiza usalama na urahisi wa matumizi akisema, “Usalama upo kwenye miamala ya kidijitali, na Lipa Chapchap inatoa uthibitisho wa miamala kwa wakati halisi, kuhakikisha wateja na wafanyabiashara wanafurahia uzoefu usio na wasiwasi. Kwa kuchanganua haraka tu, malipo yanachakatwa mara moja—hakuna haja ya kushughulika na fedha taslimu au kutumia kadi yako. Ni salama, rahisi, na imeundwa kwa urahisi kwa kila mtu”.
Kwa wateja, Lipa Chapchap inatoa huduma kwa uharaka, usalama, na kidijitali zaidi, kuwaruhusu kufanya malipo wakati wowote, mahali popote, kwa simu zao za mkononi tu. Kwa wafanyabiashara, inatoa suluhisho bila gharama yoyote ili kurahisisha miamala, kuboresha usimamizi wa mtiririko wa fedha, na kumridhisha mteja wake.
Kwa upande wake, Stanley Kafu, Mkuu wa Masoko na Mawasiliano, amesisitiza jukumu la Benki ya Exim katika kuendesha mabadiliko ya kidijitali katika sekta ya kifedha nchini.
“Kama taasisi ya kifedha inayofikiria mbele, tumejizatiti kutumia teknolojia kutoa suluhisho bunifu na zinazofaa wateja. Lipa Chapchap ni ushahidi wa kujikita kwetu kuleta mabadiliko ya kidijitali na uwezeshaji wa kifedha. Kwa kuondoa vikwazo kwa malipo ya kidijitali, hatutoi tu bidhaa—tunaunda mustakabali wa huduma za benki,” alisema Kafu.
Uzinduzi wa Lipa Chapchap ni hatua muhimu katika safari ya kidijitali ya Benki ya Exim, kuhakikisha wafanyabiashara na watu binafsi wananufaika na uzoefu wa malipo usio wa kifani, usiotumia fedha taslimu, na wenye ufanisi mkubwa.