Faida 5 za kulia usizozijua

0
31

Wengi hufikiri kulia ni jambo la kujifedhehesha na kuonekana mdhaifu.

Wataalamu wanasema, kitendo cha kulia kina faida nyingi kiafya na pia hukuondoa katika hatari ya kupata maradhi.

Hizi ni faida 5 za kulia;

1. Huondoa sumu mwilini
Kulia kunaweza kupunguza viwango vya cortisol mwilini ambavyo vinaweza kupunguza mfadhaiko wako. Kwa hivyo, wakati ujao unapopata mawazo kwa sababu ya kazi yako au masuala yako ya kibinafsi, unaweza kulia.

2. Huondoa maumivu ya hisia
Moja ya njia za asili za kupunguza maumivu ya kihisia ni kulia. Wanasayansi wamefanya tafiti juu ya kilio ambayo ilionesha kuwa kulia kunaweza kutoa neurotransmitters kwenye ubongo ambayo inaweza kupunguza maumivu ya kihemko.

3. Inaboresha macho
Machozi yana uwezo wa kulainisha kope zako na mboni za macho. Ukosefu wa maji mwilini ni moja ya sababu za kawaida za kuzorota kwa macho. Lakini, machozi yanaweza kutatua tatizo hili. Inajulikana kuwa vumbi linaweza kusababisha matatizo ya macho, lakini machozi yana uwezo wa kuondoa chembe za vumbi kwenye jicho lako.

Machozi pia yanaweza kunyunyiza utando wa mucous ulio karibu na macho.

4. Kuboresha ‘mood’ yako
Machozi yanaweza kuboresha hali ya mtu na kumfanya mtu ajisikie vizuri. Kulia inachukuliwa kama mbinu ya kujifariji. Watu walio na matatizo yanayohusiana na hisia au masuala ya wasiwasi wanaweza kujaribu kulia.

5. Huboresha mfumo wa kinga
Watu wanaokabiliwa na athari za mzio, watu walio na ukurutu na matatizo mengine ya ngozi, wanaweza kutumia kilio kama njia ya asili ya kuzuia athari za mzio. Watu wanaosumbuliwa na arthritis ya rheumatoid, ugonjwa wa autoimmune, wanaopumua kwa shida na dalili nyingine, Kulia kunaweza kudhibiti kemikali za kinga ambazo zinajulikana kuzidisha dalili za mzio.