Mambo 6 yatakayobadilika baada ya kifo cha Malkia Elizabeth II

0
22

Septemba 8 mwaka huu, baada ya kuishi kwa miaka 96, na kukaa madarakani kwa miaka 70, Malkia wa Uingereza, Elizabeth II alifariki duniani.

Kifo hicho kilitoa nafasi kwa mwanae mkubwa wa kiume, Charles Philip kuwa Mfalme wa Uingereza akitambulika kama Mfalme Charles III.

Kutokana na mabadiliko hayo, vitu vingi nchini Uingereza na nchi nyingine zilizo chini ya mfumo wa utawala wa Uingereza pamoja na Jumuiya ya Madola vitabadili ili kuashiria kukoma kwa utawala wa malkia na kuanza kwa utawala wa mfalme.

Hapa chini ni baadhi tu ya vitu hivyo;

Bendera

Kuanzia bendera zinazopepea nje ya vituo vya polisi kote Uingereza hadi kwenye meli ya jeshi la maji, maelfu ya bendera zilizo na alama za EIIR zitahitajika kubadilishwa.

Charles atahitaji bendera mpya ya binafsi kama Mfalme. Mnamo 1960 Malkia alipitisha bendera binafsi – E ya dhahabu na taji ya kifalme ambayo ilitumika mara nyingi alipotembelea nchi za Jumuiya ya Madola. Bendera ya Malkia ilikuwa ni kwaajili yake pekee, na hakutakiwa mtu yeyote kuipeperusha isipokuwa yeye.

Noti za benki na sarafu

Kuna noti za benki paundi bilioni 4.5 zinazosambazwa zikiwa na uso wa Malkia. Kuzibadilisha kwenye sura ya mfalme mpya kuna uwezekano kuchukua angalau miaka miwili.

Wimbo wa taifa

Moja ya mabadiliko yatakuwa kubadilisha maneno ya wimbo wa taifa kutoka “Mungu Mlinde Mtukufu Malkia” hadi “Mungu Mlinde Mtukufu Mfalme.”

Maombi

Malkia alikuwa “mlinzi wa imani na gavana mkuu” wa Kanisa la Anglikana, na kuna sala kwa ajili yake katika kitabu cha maombi . Haya yanatarajiwa kurekebishwa na kuwa maombi ya mfalme mpya.

Ahadi za utii

Tangu 1952 maneno yamekuwa haya; “mimi (jina la mwanachama) naapa kwa Mwenyezi Mungu kwamba nitakuwa mwaminifu na kuwa mwaminifu wa kweli kwa ukuu wake Malkia Elizabeth, warithi na warithi wake kwa mujibu wa sheria. Mungu nisaidie.”

Wabunge na wengine watalazimika kuapisha kiapo kipya kwa mrithi wake.

Jumuiya ya Madola

Nchi 14 ambazo zinamtambua mfalme kama mkuu wa nchi, katiba zao zinasema kwamba Malkia haswa ndiye mkuu wa nchi. Katika nchi hizi, katiba zitahitaji kurekebishwa ili kumtambua mrithi wake.

Aidha, kunauwezekano wa baadhi ya nchi zilizo chini ya mfumo wa Uingereza kutaka kujitoa na kuwa na uongozi wake unaojitegemea. Hadi anafariki dunia, malkia alikuwa kiongozi wa nchi 15.