Mfahamu Charles III, Mfalme ajaye wa Uingereza

0
20

Charles III ( Charles Philip Arthur George) alizaliwa Novemba 14, 1948 katika jumba la Buckingham kama mjukuu wa kwanza wa Mfalme George VI.

Alisoma katika shule za Cheam na Gordonstoun, ambazo baba yake alisoma akiwa mtoto. Baadaye alikaa mwaka mmoja katika Chuo Kikuu cha Timbertop cha Shule ya Geelong Grammar huko Victoria, Australia.

Baada ya kupata Shahada ya Sanaa kutoka Chuo Kikuu cha Cambridge, Charles alihudumu katika Jeshi la Anga la Kifalme na Jeshi la Wanamaji la Kifalme kutoka 1971 hadi 1976.

Mnamo 1981, alimuoa Lady Diana Spencer, ambaye alizaa naye watoto wawili Prince William na Prince Harry na baadaye walitengana na kumuoa Camilla Parker Bowles mnamo 2005.

Alikuwa mwanamfalme aliyehudumu kwa muda mrefu zaidi akiwa ameshikilia cheo hicho kuanzia Julai 26, 1958 hadi kutawazwa kwake Septemba 8, 2022 kufuatia kifo cha mama yake, Elizabeth II.

Sasa anatazamiwa kuwa mfalme wa Uingereza na maeneo mengine 14 ya Jumuiya ya Madola.

Send this to a friend