Miili ya watu watatu yafukuliwa nyumbani kwa mganga wa kienyeji, saba wakamatwa

0
31

Jeshi la Polisi linawashikilia watu saba akiwemo mganga wa kienyeji, Nkamba Kasubi kwa kosa la mauaji ya watu watatu ambao wanadaiwa kuuawa na kufukiwa nyumbani kwa mganga huyo mkoani Singida.

Kati ya miili hiyo, miwili imetambuliwa ambapo mmoja ni wa Gedion Samwel Mnyawi (53), aliyeuawa baada ya kuwauzia shamba mara mbili Hawa Hussein Sumwa (54) na Idd Hussein Idd (25) wote wakiwa wakazi wa Makuro.

Akitoa taarifa hiyo, Msemaji wa Jeshi la Polisi, David Misime amesema baada ya watu hao kuuziwa shamba hilo mara mbili na baadaye kugundua kuwa shamba hilo tayari liliuzwa kwa mtu mwingine, walikwenda kwa mganga huyo ambaye aliwaambia kuwa ili pesa zao zirudi inabidi mwanaume huyo atolewe kafara.

“Mabaki ya mili ya watu hao wawili yamebainika baada ya wananchi na Askari kuoneshwa na Asha Bakari (51) mkazi wa Migugu ambaye ni mke wa Awadh Ramadhani maarufu Wawa (54 ) ambao ni wakwe wa Nkamba Kasubi mganga wa kienyeji ambao walikamatwa,” imeeleza taarifa.

Send this to a friend