Nchi 10 za Afrika zenye bei ya Juu zaidi ya mafuta kwa Septemba

0
16

Tangu mwanzo wa mwaka huu, ulimwengu umekutana na changamoto za kiuchumi ambazo zina athari kubwa kwa wananchi wa kawaida. Viwango vya mabadiliko ya bei na mfumuko wa bei ambao unabadilika mara kwa mara unazua wasiwasi na utata kwa umma, na mambo kadhaa yanaweza kuchangia hali hiyo, ikiwa ni pamoja na mivutano ya kijiopolitiki, mabadiliko katika mahitaji na ugavi wa bidhaa, na mambo mengineyo.

Uchumi wa Afrika, kama maeneo mengine, umekuwa dhaifu kutokana na sababu za kiuchumi ambazo zinaweza kuwa na athari nzuri au mbaya kwa maendeleo ya bara hilo. Moja ya sababu hizo ni gharama ya nishati, ambayo kwa kawaida ina athari kubwa katika viwanda vingi.

Nchi 10 zenye uwekezaji mkubwa kutoka nje

Baadhi ya uchumi unaoendelea barani Afrika hauwezi kuhimili athari za kiuchumi zinazotokana na kuongezeka kwa gharama za nishati, na hivyo kufanya bei ya petroli ionekane kuwa ghali sana. Nchi kadhaa za Afrika zinauza mafuta kwa bei chini ya bei ya wastani ya dunia ya $1.33 [TZS 3,332] kwa lita, lakini bado zinaathiriwa sana na ongezeko la bei ya mafuta.

Orodha hii imeandaliwa na GlobalPetrolPrices.com, jukwaa ambalo linasasisha bei za mafuta kila siku duniani kote. Bei hizi ni kwa shilingi ya Tanzania;

Afrika ya Kati: 4,505
Malawi: 4,129
Senegal: 4,054
Zimbabwe: 4,034
Seychelles: 3,973
Mauritius: 3,788
Cape Verde: 3,778
Morocco: 3,690
Zambia: 3,595
Mali: 3,547
Chanzo: Business Insider

Send this to a friend