Nchi 10 za Afrika zinazoongoza kwa ndoa za wake wengi

0
17

Ndoa za mke zaidi ya mmoja au mitala zimepigwa marufuku katika sehemu nyingi duniani, na hata Kamati ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa imeeleza kuwa inakiuka heshima ya wanawake na kuitaka iondolewe kabisa popote inapoendelea kuwepo.

Katika nchi nyingi, ndoa zinasimamiwa na sheria za kidini au desturi za kawaida, ambayo inamaanisha kuwa uangalizi unakuwa mikononi mwa viongozi wa dini au viongozi wa jamii.

Takwimu za hivi karibuni zinaonyesha kuwa viwango vya ndoa za mke zaidi ya mmoja ni vya juu katika sehemu za Magharibi na Kati mwa Afrika, ambapo bado ni halali.

Pia, mitala ina tabia ya kutofautiana kulingana na imani ya kidini.

Hizi hapa ni nchi 10 za Kiafrika zilizo na viwango vya juu zaidi vya ndoa za mitala, kulingana na takwimu kutoka Kituo cha Utafiti cha Pew.

1. Burkina Faso: 36%
2. Mali: 34%
3. Gambia: 30%
4. Niger: 29%
5. Nigeria: 28%
6. Guinea:26%
7. Guinea-Bissau:23%
8. Senegal: 23%
9. Togo: 17%
10. Chad: 15%

Send this to a friend