
FILE PHOTO: The hands of a patient with skin rashes caused by the mpox virus are pictured at the treatment center of Vijana Hospital in Kinshasa, Democratic Republic of Congo August 30, 2024. REUTERS/Justin Makangara/File Photo
Wizara ya Afya imetangaza kumalizika kwa ugonjwa wa Virusi vya Marburg (MVD) nchini .
Taarifa iliyotolewa na Wizara ya Afya imesema wagonjwa wawili walithibitika kuwa na maambukizi mkoani Kagera, ambapo kwa bahati mbaya wagonjwa hao walifariki wakati wakipatiwa matibabu.
“Kitaalamu na kulingana na kanuni na taratibu za Shirika la Afya Duniani (WHO), tumekidhi vigezo vya kutangaza rasmi kumalizika kwa mlipuko wa MVD. Hivyo basi, leo Machi 13, 2025, ninatangaza rasmi kumalizika kwa mlipuko wa MVD nchini, imesema taarifa iliyotolewa na Waziri Jenista Mhagama.
Aidha, Taarifa hiyo imeisisitiza jamii yote kuendelea kuwa makini hata baada ya kutangazwa kumalizika kwa mlipuko huo kwa kuzingatia hatua zote za kujikinga , ikiwa ni pamoja na kunawa mikono kwa maji tiririka na sabuni, au kutumia vitakasa mikono (sanitizer).