Tanzania yashika nafasi ya 6 kwa utawala bora Afrika 2025

0
137

Utawala bora unaendelea kuwa kipengele muhimu kinachoamua mwelekeo wa maendeleo, uthabiti wa kiuchumi na mshikamano wa kijamii katika nchi za Afrika.

Kwa mujibu wa Country Governance and Government Index (CGGI), tathmini ya kila mwaka inayopima serikali 120 duniani, zaidi ya nusu ya nchi hizo zimeonesha kuporomoka kwa viwango vyao vya utawala kati ya mwaka 2021 na 2025.

CGGI hupima uwezo wa serikali katika utekelezaji wa sera, ufanisi wa taasisi na uwajibikaji wa umma, na kutoa taswira ya kina juu ya jinsi serikali zinavyokidhi mahitaji ya wananchi wake.

Kwa upande wa Tanzania, ripoti hii imeitaja kuwa miongoni mwa nchi zenye utawala bora barani Afrika mwaka 2025, ambapo imeshika nafasi ya 6 Afrika na nafasi ya 78 duniani.

Hizi ni nchi 10 za Afrika zenye utawala bora mwaka 2025;

1 Mauritius
2 Rwanda
3 Botswana
4 Morocco
5 Afrika Kusini
6 Tanzania
7 Misri
8 Senegal
9 Ghana
10 Namibia

Chanzo: Business Insider Africa

Send this to a friend