TCC Plc. yaweka rekodi kwa kuongeza faida mara mbili zaidi

0
13

Dar es Salaam, Aprili 26, 2023, Kampuni ya Tanzania Cigarette Public Limited (TCC Plc) imeweka rekodi ya mauzo ya mwaka 2022, kutokana na mbinu za kina na mkakati zilizowekwa na kampuni, pamoja na ushirikiano thabiti ndani ya kampuni.

Mwenyekiti wa Bodi ya TCC Plc, Paul Makanza, ameweka wazi mafanikio hayo makubwa ya kampuni leo, wakati akizungumza na wanahisa na wadau wa kampuni jijini Dar es Salaam katika mkutano mkuu wa mwaka.

Mwenyekiti wa TCC, Bw. Paul D Makanza akizungumza na Wanahisa wa TCC wakati wa Mkutano Mkuu wa 58 unaofanyika jijini Dar es salaam.

Makanza amepongeza utendaji wa TCC kwa ukuaji imara ambao umepelekea mtiririko thabiti wa fedha za uendeshaji na ongezeko la thamani ya wanahisa kwa mwaka wa tatu mfululizo.

Katika taarifa yake, Paul alisema, “Kwa upande wa matokeo yetu ya fedha, nina furaha kuripoti kwamba faida yetu kabla ya kodi (PBT) kwa mwaka iliongezeka kwa asilimia 23.7 ambayo ni sawa na TShs bilioni 106.8, ikilinganishwa na TShs. 86.3 bilioni za mwaka 2021.

Amesema ingawa kodi ya mapato iliongezeka kwa asilimia 40.2 kutokana na marekebisho ya kodi ya mapato ya miaka ya awali, faida baada ya kodi (PAT) bado ilionyesha ongezeko kubwa la asilimia 16.2 hadi kufikia TShs. bilioni 69.2 kutoka TShs. bilioni 59.6 mwaka wa 2021.

Ukuaji huu wa faida ulichangiwa na ufanisi sahihi wa kiutendaji na usimamizi mzuri wa gharama.

Kulingana na taarifa ya Mkurugenzi Mtendaji na Meneja Mkuu, Takashi Araki, amesema kiasi cha ndani kilifikia bilioni 5.7 katika kipindi hicho, ambacho kilikuwa ni ongezeko la asilimia 10 kutoka 2021.

Mkurugenzi Mtendaji, Takashi Araki akizungumza katika Mkutano Mkuu wa 58 wa TCC kwenye Hoteli ya Hyatt Regency.

Zaidi ya hayo, alibainisha, kiasi cha juu kabisa cha kampuni kuwahi kutengeneza kilifikia bilioni 9 ambapo faida yake ilikua kwa mara mbili zaidi.

Araki alihusisha siri za mafanikio ya kampuni na rasilimali watu, akisema; “Wafanyakazi wetu waliojitolea wamekuwa rasilimali yetu kubwa, na kuiwezesha TCC Plc kutambuliwa kama mwajiri mkuu nchini Tanzania na Afrika kwa miaka mitano mfululizo. Tutaendelea kuwekeza kwa watu wetu na kukuza mazingira jumuishi na yenye usalama mahali pa kazi.”

Pia alipongeza juhudi za Serikali kwa kuweka mazingira ya kuaminika na rafiki kwa biashara ambayo ni pamoja na kutoa motisha kwa matumizi ya tumbaku inayopatikana nchini na kuimarika kwa ushuru wa bidhaa ulioiwezesha kampuni kuboresha soko lake.

Kuhusu uendelevu wa kijamii, Araki alieleza: “Uendelevu ni kipaumbele cha msingi katika TCC Plc. Tumefanya juhudi nyingi za kulinda mazingira, kufanya kazi kwa uwajibikaji, na kuhakikisha utawala bora, ikiwa ni pamoja na uwekezaji katika miradi ya nishati ya jua, maji na usimamizi wa taka.

Wanahisa wa TCC, Wajumbe wa Bodi, Uongozi na Wageni Waalikwa