TFF kukagua mikataba ya timu za Ligi Kuu

0
12

Kamati ya Leseni za Klabu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imeanza ukaguzi wa klabu za Ligi Kuu, ukaguzi utakaofanyika katika maeneo ya mpango kazi wa timu za vijana, hati ya umiliki wa uwanja au mkataba wa upangaji.

Pia, Sekretarieti ya klabu (structure) pamoja na mikataba ya wafanyakazi/benchi la ufundi, katiba pamoja na cheti cha usajili (Halisi na nakala) na hesabu za fedha zilizokaguliwa za mwaka 2021.

TFF yaijibu Yanga: Hatuhusiki kualika wageni Mkutano Mkuu wa CAF

Kwa mujibu wa taarifa, klabu zote tayari zimepewa taarifa, ikiwemo tarehe ya ukaguzi pamoja na maandalizi wanayotakiwa kufanya.

Send this to a friend