Utafiti: Kahawa, chai nyingi kwa mjamzito husabababisha kujifungua kabla ya wakati

0
19

Utafiti uliochapishwa katika Jarida la Kimataifa la Epidemiology umebaini kwamba unywaji wa kafeini nyingi na uvutaji wa sigara kwa mama mjamzito ni hatari zaidi kwa mtoto.

Huduma ya Afya ya Taifa (NHS) inapendekeza wanawake wajawazito wasinywe zaidi ya 200mg ya kafeini kwa siku, sawa na vikombe viwili vya kahawa au chai pamoja na kuepuka uvutaji wa sigara.

Hii ni kwa sababu kunywa kiasi kikubwa cha kafeini na kuvuta sigara vimehusishwa na hatari zaidi ya matatizo wakati wa ujauzito, kujifungua kabla ya wakati, na upungufu wa ukuaji wa kiumbe tumboni.

Kwa upande mwingine, utafiti umebaini kwamba wanawake wanaovuta sigara wakati wa ujauzito walikuwa karibu mara tatu zaidi kujifungua mtoto njiti ikilinganishwa na wasiovuta sigara.

Pia uligundua kwamba watoto wanaozaliwa na mama ambao walivuta sigara walikuwa na hatari mara nne zaidi ya kuwa na changamoto ya ukuaji kulingana na athari zilizotengenezwa wakati wa ujauzito, ambao uliwaweka katika hatari ya matatizo makubwa ikiwa ni pamoja na matatizo ya kupumua na maambukizo.