Watu 10 matajiri zaidi Afrika mwaka 2024

0
39

Kuna idadi kubwa ya mabilionea wa Kiafrika ambao ni wajasiriamali matajiri sana kutokana na mafanikio yao katika biashara na sekta mbalimbali.

Matajiri hawa wamekuwa kichocheo kikubwa cha uchumi wa bara la Afrika kutokana na mchango mkubwa wanaoutoa, lakini pia wamekuwa kioo hasa kwa vijana wanaopambana kutimiza ndoto zao.

Kwa kuelekeza utajiri wao katika mipango ya kimkakati, watu hawa wanaweza kukuza ukuaji wa uchumi, kukuza ustawi wa jamii, na kusukuma bara kuelekea mustakabali endelevu na unaojumuisha watu wote.

Hapa chini ni matajiri 10 barani Afrika katika mwanzo wa mwaka 2024 (TZS);

  1. Johann Rupert & Familia (Afrika Kusini): Trilioni 25.8
  2. Aliko Dangote (Nigeria): Trilioni 23.8
  3. Nicky Oppenheimer & Familia (Afrika Kusini): Trilioni 20.8
  4. Nassef Sawiris (Misri): Trilioni 18.5
  5. Abdulsamad Rabiu (Nigeria): Trilioni 14.7
  6. Nathan Kirsh (Swaziland): Trilioni 14.5
  7. Issad Rebrab & Familia (Algeria): Trilioni 11.5
  8. Mohamed Mansour (Misri): Trilioni 9
  9. Naguib Sawiris (Misri): Trilioni 8.2
  10. Mike Adenuga (Nigeria): Trilioni 7.8
Send this to a friend