in ,

Viwanja 10 Tanzania vilivyoingiza mapato zaidi msimu wa 2020/21

Wakati pazia la msimu mpya wa mwaka 2021/25 likifunguliwa mwishoni mwa mwezi huu, vilabu vimeendelea kuweka mikakati ya kukusanya mapato ili kuendesha shughuli zao.

Makusanyo ya getini kwenye viwanja vya mpira wa miguu nchini ni moja ya vyanzo vikubwa vya mapato kwa vilabu vya soka nchini, lakini kiwango cha makusanyo ya getini kinatofautiana kutoka kiwanja kimoja hadi kingine.

Hapa chini ni orodha ya viwanja 10 vilivyoingiza fedha zaidi msimu uliopita kati ya viwanja 21 vilivyotumika kwenye mashindano mbalimbali.

1. Uwanja wa Benjamin Mkapa (Dar es Salaam) – Bilioni 1.9


2. Uwanja aa Jamhuri (Dodoma) – Milioni 287.3


3. Uwanja wa Sokoine(Mbeya) – Milioni 227.05


4. Uwanja wa CCM Kirumba (Mwanza)- Milioni 191.9


5. Sheikh Amri Abeid (Arusha)- Milioni 122.7


6. Uwanja wa Jamhuri (Morogoro)- Milioni119.8


7. Uwanja Kambarage (Shinyanga)- Milioni 115.9


8. Uwanja wa Gwambina (Mwanza)- Milioni 114.6


9. Uwanja wa Nelson (Rukwa)- Milioni 80.9


10. Azam Complex-Chamazi (Dar es Salaam)- Milioni 72.99

Rais Samia aunda timu ya kuandaa mkakati wa kuwainua wanawake

Yanga kinara wa mapato msimu wa 2020/21