in , , ,

Nchi 10 za Afrika zenye kiwango kikubwa cha wasiojua kusoma na kuandika

Kutokujua kusoma na kuandika kunaweza kuwa na athari kubwa kwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii ya nchi. Watu wasiojua kusoma na kuandika wanaweza kukabiliwa na vizuizi vingi katika kupata elimu, fursa za ajira, na hata kushiriki katika shughuli za kijamii na kisiasa.

Sababu zinazochangia viwango vya chini vya usomaji na uandishi ni pamoja na upungufu wa miundombinu ya elimu, upatikanaji mdogo wa vitabu na vifaa vya kusomea, umaskini, migogoro ya kisiasa na kijamii, na mifumo ya elimu ambayo haiwezi kukidhi mahitaji ya wananchi wake.

Nchi 10 za Afrika zinazoongoza kwa joto kali

Hizi ni nchi 10 za Kiafrika zenye viwango vya juu vya watu wasiojua kusoma na kuandika;

Ivory Coast: 43.27%
Chad: 40.02%
Benin: 38.45%
Somalia: 37.80%
Burkina Faso: 37.75%
Jamhuri ya Afrika ya Kati: 36.75%
Mali: 33.07%
Sudan Kusini: 31.98%
Guinea: 30.47%
Niger: 19.10%

Dereva wa ajali iliyoua wanafunzi Arusha ashtakiwa kwa kuua bila kukusudia

Rais Samia kutunukiwa Udaktari wa Heshima na Chuo Kikuu cha Ankara, Uturuki